Stars,Tunisia Zagawana Pointi |Shamtee.blog

Timu ya Taifa ya Tanzania(Taifa Stars) imegawana alama na Tunisia baada ya kutoka sare ya 1-1 katika mchezo wa ligi kuu uliofanyika jijini Dar es salaam.

Tunisia walianza kumiliki mchezo tangu dakika ya 1 na kufanikiwa kupata bao la uongozi dakika ya 11 baada ya walinzi wa Stars kujichanganya na kumuacha pekee Salf-Eddine Khaoui aliyefunga bao zuri huku kipa Aishi Manula akijaribu kuokoa bila mafanikio.

Taifa Stars walirudi mchezo baada ya kuingia kwa Feisal Salum ambaye dakika ya 47 alifunga bao la kusawazisha kwa shuti kali bao ambalo lilidumu mpaka mwisho wa mchezo.

Tunisi wamekaa kileleni kwa alama tisa huku Equatorial Guinnea wakiwa nafasi ya pili kwa alama 6 huku Stars wakiwa na alama 4 nafasi ya pili a Libya wakishikika mkia katika msimamo wa kundi J.

The post Stars,Tunisia Zagawana Pointi appeared first on Sports Leo.



By Author

0/Post a Comment/Comments

Previous Post Next Post