WHO:Chanjo isitarajiwe kutokomeza kabisa virusi vya corona |Shamteeblog.

Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO) limesisitiza kwa mara nyingine tena kwamba inahitajika asilimia 60 mpaka 70 ya watu wapatiwe chanjo ili kupatikane kuwepo kinga dhidi ya maambukizi ya virusi vya corona kwa makundi ya watu.

WHO limesema kwa namna hiyo mafanikio mazuri yataweza kupatikana katika mapambano dhidi ya janga hilo. Mratibu wa misaada ya dharura wa shirika la WHO,Mike Ryan amesema hata hivyo chanjo hiyo isitarajiwe kutokomeza kabisa virusi vya corona.

Amesema ili kufikia kiwango hicho wanasayansi watahitaji kufanya utafiti zaidi juu ya utaratibu mzima wa virusi vya SARS-CoV-2 vinavyosababisha ugonjwa wa COVID -19.



from Author

0/Post a Comment/Comments

Previous Post Next Post