🟢HAWA NDIYO WASHINDI UCHAGUZI WA MADIWANI VITI MAALUM CCM TARAFA MANISPAA YA SHINYANGA |Shamteeblog.

Msimamizi wa Uchaguzi, Katibu wa Vijana CCM Mkoa wa Shinyanga,Salama A. Mhampi akitangaza matokeo

Na Mwamvita Issa - Shinyanga

Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Shinyanga Mjini kimeendesha uchaguzi wa ndani wa madiwani wa viti maalum kwa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga, katika Tarafa mbalimbali, ambapo wanachama walijitokeza kwa wingi kushiriki mchakato huo muhimu uliofanyika Julai 20, 2025.


🔸 TARAFA YA MJINI

Jumla ya wagombea: 18
Kura zilizopigwa: 763
Kura halali: 751
Kura zilizoharibika: 12
Idadi ya viti vinavyogombewa: 5

Washindi waliopatikana ni:
🔹 Moshi Husein Kanji – Kura 536
🔹 Ester Festo Makune – Kura 445
🔹 Veronica E. Masawe – Kura 431
🔹 Mwanakhamis Kazoba – Kura 355
🔹 Eunice Z. Manumbu – Kura 272


🔸 TARAFA YA OLD SHINYANGA

Jumla ya wagombea: 3
Kura zilizopigwa: 554
Kura halali: 553
Kura zilizoharibika: 1
Idadi ya mshindi: 1

Mshindi aliyepatikana:
🔹 Mwanaidi Abdul Sued – Kura 539


🔸 TARAFA YA IBADAKULI (ZUHURA)

Jumla ya wagombea: 3
Kura zilizopigwa: 759
Kura halali: 758
Kura zilizoharibika: 1
Idadi ya mshindi: 1

Mshindi aliyepatikana:
🔹 Zuhura Waziri Mwambashi – Kura 695


Mchakato mzima wa uchaguzi ulifanyika kwa amani na uwazi, ambapo wanachama walionyesha mshikamano na utayari wa kuendelea kujenga chama chao kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.

Ushindi wa wagombea hawa ni ushahidi wa imani kubwa waliyonayo wanachama kwao, huku wakiahidi kuendeleza sera na mwelekeo wa CCM katika kuwatumikia wananchi kwa bidii na uadilifu.


🖊️ Imeandaliwa na – Mwamvita Issa



By Mpekuzi

0/Post a Comment/Comments

Previous Post Next Post