
Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Shinyanga Mjini kimeendesha uchaguzi wa ndani wa madiwani wa viti maalum kwa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga, katika Tarafa mbalimbali, ambapo wanachama walijitokeza kwa wingi kushiriki mchakato huo muhimu uliofanyika Julai 20, 2025.
🔸 TARAFA YA MJINI
✅ Jumla ya wagombea: 18
✅ Kura zilizopigwa: 763
✅ Kura halali: 751
✅ Kura zilizoharibika: 12
✅ Idadi ya viti vinavyogombewa: 5
Washindi waliopatikana ni:
🔹 Moshi Husein Kanji – Kura 536
🔹 Ester Festo Makune – Kura 445
🔹 Veronica E. Masawe – Kura 431
🔹 Mwanakhamis Kazoba – Kura 355
🔹 Eunice Z. Manumbu – Kura 272
🔸 TARAFA YA OLD SHINYANGA
✅ Jumla ya wagombea: 3
✅ Kura zilizopigwa: 554
✅ Kura halali: 553
✅ Kura zilizoharibika: 1
✅ Idadi ya mshindi: 1
Mshindi aliyepatikana:
🔹 Mwanaidi Abdul Sued – Kura 539
🔸 TARAFA YA IBADAKULI (ZUHURA)
✅ Jumla ya wagombea: 3
✅ Kura zilizopigwa: 759
✅ Kura halali: 758
✅ Kura zilizoharibika: 1
✅ Idadi ya mshindi: 1
Mshindi aliyepatikana:
🔹 Zuhura Waziri Mwambashi – Kura 695
Mchakato mzima wa uchaguzi ulifanyika kwa amani na uwazi, ambapo wanachama walionyesha mshikamano na utayari wa kuendelea kujenga chama chao kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.
Ushindi wa wagombea hawa ni ushahidi wa imani kubwa waliyonayo wanachama kwao, huku wakiahidi kuendeleza sera na mwelekeo wa CCM katika kuwatumikia wananchi kwa bidii na uadilifu.
🖊️ Imeandaliwa na – Mwamvita Issa
By Mpekuzi
Post a Comment