WAWILI WAKWAMA WAKATI WA TENDO, MAMIA WAJITOKEZA KUSHUHUDIA |Shamteeblog.


Kizazaa kilizuka baada ya mwanaume mmoja na mwanamke waliodaiwa kuwa katika uhusiano wa siri kukwama wakati wa tendo la ndoa. Tukio hilo lilijiri majira ya alfajiri kwenye nyumba ya kulala wageni iliyo karibu na soko kuu, na liliwavutia mamia ya wakazi waliokusanyika kushuhudia kisa hicho kisicho cha kawaida.

Mashuhuda wanasema kwamba kelele za maumivu kutoka chumbani ziliwashtua wahudumu wa hoteli, ambao walipojaribu kuingia ndani walikuta mlango umefungwa kwa ndani. Ilibidi wavunje mlango, ndipo wakawakuta wawili hao wakiwa wamelala uchi na wakilia kwa uchungu, wakiwa wamekamatana na kushindwa kutengana hata walipojaribu kujitoa kwa nguvu.


By Mpekuzi

0/Post a Comment/Comments

Previous Post Next Post