Twiga Stars(U17) Inajipigia Tu |Shamtee.blog

Timu ya Taifa ya Wanawake chini ya umri wa miaka 17 imeibuka na ushindi mnono wa mabao 10-0 dhidi ya timu ya Zimbabwe katika michuano ya Cosafa inayofanyika nchini Afrika ya Kusini.

Mabao ya Tanzania yalifungwa na Mohame aliyetupia mabao mawili dakika ya 18 na 89 huku mengine yakifungwa na Protasia Kipaga dakika ya 1,Koku Kipanga dakika ya 11, Irene Kisisa dakika 13, Ester Mabaza dakika ya 32.

Zawadi Athuman dakika ya 55, Asha Masaka naye alitupia mawili dakika ya 71 na 82, Rudo Machadu alitupia dakika ya 79 kwa upande wa Zimbabwe na kufanya liwe bao lao pekee la kufutia machozi.

Tanzania sasa imeingia katika hatua na fainali na inatarajiwa kumenyana na Zambia leo novemba 11 katika mchezo unaotarajiwa kuwa mgumu na wenye msisimko.

The post Twiga Stars(U17) Inajipigia Tu appeared first on Sports Leo.



By Author

0/Post a Comment/Comments

Previous Post Next Post