NAIBU WAZIRI ARIDHISHWA UJENZI WA BWENI NA BWALO NAMTUMBO |Shamteeblog.

NA YEREMIAS  NGERANGERA…NAMTUMBO

Naibu waziri  ofisi ya Raisi TAMISEMI  David Silinde ameridhishwa  na ujenzi  wa bweni  katika shule ya sekondari  Selous  na ujenzi wa bwalo katika shule ya sekondari  Nasuli  baada ya kufanya ziara ya kukagua  ujenzi huo na kuridhishwa  na hatua za ujenzi  wa majengo hayo na kiasi cha fedha kilichotumika .

“Nampongeza  mkuu wa wilaya  Namtumbo kwa usimamizi thabiti,nawapongeza wakuu  wa shule kwa kuwa fedha hizo za ujenzi zinafika moja kwa moja katika shule na kusimamia utaratibu wa ujenzi  hatua kwa hatua ,nawapongeza  wataalamu  wa Halmashauri  wakiongozwa  na mkurugenzi wa Halmashauri  pamoja na mkuu wa idara ya elimu sekondari  kwa kufuatilia hatua kwa hatua ujenzi huo”  alisema naibu waziri huyo.

Mkuu  wa shule ya sekondari  Selous  bwana Bernard  Nyoni  pamoja  na kuishukuru serikali  ya Raisi John Pombe Magufuli  kwa kutoa fedha milioni 80 ili kujenga bweni  kuwasaidia  wanafunzi  waliokuwa wanatembea umbali mrefu kufika shuleni  na mara kadhaa wanafunzi hao walikuwa wanakumbana  na hatari kubwa ya kuvamiwa na wanyama tembo  nyakati za asubuhi na jioni.

Nyoni  alisema  kitendo cha serikali  kuliona tatizo hilo ni ukombozi mkubwa  kwa wanafunzi  wanaosoma katika shule ya sekondari  hiyo  kwa sasa tofauti na huko nyuma  ambapo walishuhudia wazazi  wengi wakihamisha watoto wao kwenda  katika shule zingine lakini kwa sasa  wazazi wengi nao wanaomba kuwaleta watoto wao  hapa  ni matokeo ya ujenzi huu wa bweni alisema Nyoni.

Naye mkuu wa shule  ya sekondari  Nasuli  bwana Raphael  Komba  alisema shule ilipokea kiasi cha shilingi milioni 100 kwa ajili ya ujenzi wa bwalo na kadiri ya makadirio ya gharama ya ujenzi wa bwalo hilo fedha hizo hazitoshi kukamilisha ujenzi mpaka hatua za mwisho za kuanza matumizi.

 Mhandisi wa Halmashauri  ya wilaya ya Namtumbo Hassan Kinonono alidai makadirio ya gharama za ujenzi wa bwalo hilo ni milioni 150 lakini halmashuri  kupitia vikao vyake ilijitahidi kuangalia uwezekanao wa kupata fedha kutoka katika miradi mengine iliyobakiza fedha ili kuhakikisha jengo hilo linakamilika.

Mkurugenzi  wa Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo bwana  Evance  Nachimbinya alimhakikishia naibu waziri huyo kuwa Halmashauri  itahakikisha jengo hilo linaisha kwa muda uliopangwa na ofisi yake itasimamia upatikana wa fedha za kumalizia jengo hilo .



By Mpekuzi

0/Post a Comment/Comments

Previous Post Next Post