Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini, Mhe. Anord Makombe akipokea taarifa ya mradiNa Mapuli Kitina Misalaba
Kamati ya Siasa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Shinyanga Mjini imeendelea na ziara ya kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa katika Manispaa ya Shinyanga, huku viongozi wakisisitiza umuhimu wa kuhakikisha miradi hiyo inakamilika kwa wakati ili wananchi waweze kunufaika na huduma zinazotarajiwa.
Ziara hiyo imefanyika leo Machi 11, 2026 ikiongozwa na Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini, Mhe. Anord Makombe, na kuhusisha viongozi mbalimbali wa Manispaa na Wilaya.
Kamati imeanza ziara kwa kukagua ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa pamoja na matundu ya vyoo katika Shule ya Awamu na Msingi Mwengi iliyopo mjini Shinyanga ambapo Mwenyekiti Makombe amepongeza hatua za mradi huo.
Baada ya hapo, kamati imetembelea ujenzi wa zahanati katika Kijiji cha Kolandoto, Kata ya Kolandoto ambapo Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini, Mhe. Anord Makombe ameeleza kuwa zahanati hiyo ni muhimu kwa kuhakikisha wananchi wanapata huduma za afya kwa haraka na karibu na makazi yao.
Kamati pia imekagua mradi wa upanuzi wa mtandao wa majisafi unaotekelezwa na SHUWASA katika Kata ya Kolandoto na kwamba Mwenyekiti Makombe amesisitiza kuwa maji safi ni muhimu kwa afya ya wananchi na maendeleo ya kijamii, hivyo mradi lazima ukamilike kwa wakati na bila dosari za kiufundi.
Ziara ilihusisha ukaguzi wa mradi wa TANESCO wa upanuzi wa umeme katika eneo la Ibadakuli ambapo Samweli Jackson Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini amepongeza juhudi za serikali na TANESCO huku Mwenyekiti Makombe akihimiza uwajibikaji wa mara kwa mara ili mradi ukamilike kwa wakati na wananchi wapate umeme wa uhakika.
Kamati pia imetembelea Shule ya Sekondari Rajani iliyopo Kata ya Ibadakuli ili kukagua ujenzi wa mabweni mapya huku Makombe akisema mabweni ni muhimu kwa kutoa hifadhi salama kwa wanafunzi na kuhamasisha malezi bora.
Ziara hiyo imemalizika kwa kukagua ujenzi wa jengo la wahandisi katika Manispaa ya Shinyanga ambapo Mwenyekiti Makombe ameridhika na hatua ya mradi huo.
Ziara hiyo imehusisha viongozi mbalimbali: Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini Mhe. Anord Makombe; Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini Mzee Fue Mrindoko; Katibu Tawala wa Wilaya ya Shinyanga Said Kitinga; Mstahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga, Mhe. Salum Kitumbo; Kaimu Katibu wa CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini Doris Kibabi,
Samweli Jackson Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjinin a viongozi wengine wakiwemo kutoka ofisi ya mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga.
Mwenyekiti Makombe amesisitiza kuwa Kamati itaendelea kufuatilia kila mradi ili kuhakikisha malengo ya maendeleo kwa wananchi wa Manispaa ya Shinyanga yanatimizwa kwa wakati na kwa ubora unaotakiwa.
Kaimu Katibu wa CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini ambaye ni katibu wa jumuiya ya wazazi Wilaya ya Shinyanga mjini Bi. Doris Kibabi, amepongeza utekelezaji wa miradi inayotekelezwa katika Manispaa ya Shinyanga.
Doris amebainisha kuwa miradi hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa ilani ya chama cha mapinduzi (CCM) chini ya Serikali ya Awamu ya Sita ya Rais Samia Suluhu Hassan.
Amesema miradi hiyo, ikiwemo ujenzi wa madarasa, mabweni na miundombinu ya majisafi, ni ishara ya dhahiri ya ahadi za chama kufikiwa na kuleta maendeleo kwa wananchi wa Shinyanga huku akiwataka wananchi kushirikiana na viongozi kuhakikisha miradi hiyo inakamilika kwa wakati na kwa ubora unaotakiwa.
Ziara ya siku mbili ya Kamati ya Siasa ya CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini imehitimishwa leo ambapo viongozi wamesisitiza kuwa ufuatiliaji wa miradi hiyo utaendelea ili kuhakikisha kila mradi unakamilika kwa wakati, unaendana na viwango vya ubora na kwamba wananchi wanapata huduma zinazotarajiwa.
Mwalimu Mkuu wa Shule ya Awali na Msingi Mwenge Manispaa ya Shinyanga Hassan Hemed akisoma taarifa fupi ya mradi huo.
Mwalimu Mkuu wa Shule ya Awali na Msingi Mwenge Manispaa ya Shinyanga Hassan Hemed akisoma taarifa fupi ya mradi huo.
Mwalimu Mkuu wa Shule ya Awali na Msingi Mwenge Manispaa ya Shinyanga Hassan Hemed akisoma taarifa fupi ya mradi huo.
Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini, Mhe. Anord Makombe akizungumza wakati wa ziara ya kukagua mradi katika shule ya msingi Mwenge mjini Shinyanga.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini, Mzee Fue Mrindoko akizungumza.
Ziara ya kutembelea na kukagua mradi katika shule ya awali na msingi Mwenge ikiendelea.
Jengo la zahanati katika Kijiji cha Kolandoto, Kata ya Kolandoto ambapo ujenzi unaendelea.
Mwenyekiti Makombe akipokea taarifa ya ujenzi wa jengo hilo.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini, Mzee Fue Mrindoko.
Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini, Samweli Jackson akizungumza.
Katibu Tawala wa Wilaya ya Shinyanga, Said Kitinga, akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya.
Kaimu Mkurugenzi mamlaka hiyo Mhandisi Uswege Musa, akizungumza.
Kaimu Mkurugenzi mamlaka hiyo Mhandisi Uswege Musa, akisoma taarifa ya mradi huo.





Ziara ikiendelea.
Mradi wa TANESCO wa upanuzi wa umeme katika eneo la Ibadakuli.
Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini, Samweli Jackson akizungumza wakati wa ziara ya kukagua mradi wa TANESCO katika Kata ya Ibadakuli.

wenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini, Mzee Fue Mrindoko akizungumza ambapo amepongeza hatua nzuri ya mradi huo.

Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini, Mhe. Anord Makombe akipongeza weledi na kasi ya mradi huo kuwa unaridhisha.
Katibu Tawala wa Wilaya ya Shinyanga, Said Kitinga, akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya.
Mabweni mapya katika shule ya Sekondari Rajani iliyopo Kata ya Ibadakuli.

Kaimu Katibu wa CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini, Doris Kibabi akizungumza wakati wa ziara ya kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa kwa mujibu wa Ilani ya CCM.
Ziara ikiendelea.




Shule ya Sekondari Rajani iliyopo Kata ya Ibadakuli.

Mwenyekiti Makombe na kamati yake baada ya kuwasili katika mradi wa ujenzi wa jengo la wahandisi. 
By Mpekuzi
Post a Comment