Na Lydia Lugakila - Bukoba
Askofu Keshomshahara amesisitiza kuwa vifaa vya tiba vitakavyotolewa vitakuwa na uwezo wa kuchunguza magonjwa mbalimbali ya ndani ya mwili, kama vile majeraha, aina zote za kansa, utafiti wa damu iliyoganda, uchunguzi wa mifupa, na magonjwa mengine makubwa.
"Hii ni fursa kwa wakazi kazi kwa wananchi wa Mkoani Kagera kuweza kupata huduma bora za afya karibu na nyumbani," amesema mtumishi huyo wa Mungu.
Aidha, Askofu ameongeza kuwa upatikanaji wa vifaa hivi kutasaidia kuondoa changamoto za kutafuta huduma za afya katika mikoa mingine kama Mwanza na Dar es Salaam, pamoja na Nchi za nje.
Ametoa shukrani kwa serikali kwa kutoa wataalam wa kuhakiki na kuhakikisha vifaa hivyo vinafaa kwa matumizi.
Miongoni mwa vifaa vinavyotarajiwa kuzinduliwa ni pamoja na CT Scan kubwa, X-ray kubwa, Ultrasound kubwa, Digital Mammograph, pamoja na kifaa cha kuchukua picha na kutunza picha za kuwasiliana na madaktari walioko ndani na nje ya Nchi.
Tukio hili linaonyesha hatua nzuri katika kuboresha huduma za afya katika Mkoa wa Kagera, na kuleta matumaini mapya kwa wananchi wa eneo hilo.
By Mpekuzi
Post a Comment