Mbunge wa Jimbo la Singida Magharibi, Elibariki Kingu, ameonesha uongozi wa kipekee kwa kutoa msaada wa vifaa mbalimbali kwa UVCCM Mkoa wa Singida.
Katika hafla iliyofanyika Machi 24, 2025, katika Ukumbi wa RC Mission, Mkoani Singida, Kingu alikabidhi pikipiki 6 kwa makatibu wa UVCCM katika Wilaya zote sita za Mkoa wa Singida.Aidha, ametoa bati 120 yenye thamani ya milioni 3.1 kwa UWT Mkoa wa Singida na tiles za milioni 7 kwa Ofisi ya CCM Wilaya ya Ikungi. Kingu pia ametoa shilingi milioni 3 kwa Jumuiya za Wilaya ya Ikungi.
Katika hafla hiyo, Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Mohamed Kawaida, ambaye alikuwa mgeni rasmi, amekabidhi gari la jumuiya hiyo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Singida, Halima Dendego, ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati ya Siasa Mkoa. Pikipiki sita zilizotolewa na Mbunge Kingu zilikabidhiwa kwa UVCCM Wilaya ya Singida Magharibi.
Mbunge Kingu amekumbusha ahadi aliyotoa kwa vijana wa Mkoa wa Singida kwamba atawasaidia kwa vifaa vya kazi ili kuhakikisha wanapata fursa za maendeleo.
Amesisitiza kuwa, kwa kushikamana na vijana wake, ataendelea kuwaunga mkono kwa uwezo wake wote na kurejesha heshima kwa chama chake.
Kingu ameongeza kuwa aliagiza pikipiki hizo kutoka Uingereza na kusema alitumia fedha taslimu kiasi cha milioni 16.2 kwa ununuzi wa pikipiki 6, ambazo zimesajiliwa kwa jina la UVCCM na tayari zimelipiwa kodi zote.
Hafla hiyo imekamilika kwa risiti ya ununuzi wa pikipiki hizo, ambayo Kingu alikabidhi kwa Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Mohamed Kawaida, kama uthibitisho wa malipo yaliyofanywa.
By Mpekuzi
Post a Comment